Ijue ndege ya dreamliner ni ndege gani? na Mataifa mangapi yanamiliki ndege hizo.

Mataifa ya Afrika yaliyo na Dreamliner

Ethiopia (Ethiopian Airlines )*- 19
Kenya (Kenya Airways) - 8
Morocco (Royal Air Maroc) - 5
*Ethiopia pia wana Boeing B787-9 tatu, ambayo ni ndege kubwa kuliko 787-8 na inaweza kuwabeba abiria 290



Boeing 787-8 Dreamliner ni ndege ya aina gani?

Boeing 787-8 Dreamliner ni ndege ya kisasa. Bei yake inakadiriwa kuwa $224.6 milioni (Sh512 bilioni za Tanzania) kwa mujibu wa taarifa kwenye tovuti ya kampuni ya Boeing.
Ndege hiyo ya Tanzania ilisafiri kutoka uwanja wa Paine mjini Seattle, Washington safari ya umbali wa saa 22 siku ya kupokelewa kwake Julai.
Ndege hiyo hutumia injini ya kisasa zaidi aina ya Trent 1000 TEN
Injini hiyo inatumiwa katika ndege zote mpya aina ya Boeing 787 na huhifadhi mafuta, ambapo huwa inachoma mafuta kwa kiwango cha asilimia tatu chini ukilinganisha na ndege za aina hiyo na kuyatumia vyema zaidi.
Hilo huiwezesha kupunguza matumizi ya mafuta ukilinganisha na ndege nyingine za ukubwa kama wake kwa asilimia 20-25, aidha hupunguza utoaji wa gesi chafu kwa kiwango sawa na hicho.
Aidha, huwa haipigi kelele sana. Ni ndege ambayo imechukua uwezo na kasi ya ndege kubwa aina ya 'jet' na kuuweka kwenye ndege ya ukubwa wa wastani.
Ina uwezo wa kubeba abiria 262 ni ya kisasa zaidi kuwahi kumilikiwa na serikali ya Tanzania. Mataifa mengine kama vile Kenya na Ethiopia hata hivyo yamenunua ndege kama hizo kadha.



Rais Magufuli akiwa ndani ya ndege hiyoHaki miliki ya pichaIKULU
Image captionRais Magufuli akiwa ndani ya ndege hiyo

Ndege hii ina uwezo wa kusafiri kiilomita 13,620 kwa wakati mmoja na urefu wake ni mita 57. Upana wa mabawa yake ni mita 60. Urefu wake kutoka chini hadi juu ni mita 17.
Rais Magufuli aligusia hilo alipokuwa anaipokea uwanja wa wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam aliposema: "Ndege hii ni ya kisasa na kote walikopita walikuwa wana uwezo wa kunipigia simu na kuongea nao angani."



AirTanzania

Ethiopia ilikuwa nchi ya kwanza duniani kando na Japan kuanza kutumia ndege aina ya Boeing 787-8 Agosti 2012.
Ndege hiyo yenye uwezo wa kuchukua abiria 262, tayari ishaanza kutoa huduma kwa safari za ndani katika vituo vya Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mwanza.
Mwezi Septemba itaanza safari zake kwenda Bombay nchini India, Guangzhou nchini China na Bangkok nchini Thailand.

Comments

Popular Posts